iqna

IQNA

IQNA – Dar al-Ifta ya Misri imetoa fatwa mpya ya kidini inayoruhusu raia kuelekeza mali ya zakat kusaidia mahitaji ya msingi ya watu waliokoseshwa makazi huko Gaza.
Habari ID: 3481373    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/15

IQNA – Kijana mmoja wa Kipalestina amegundua nakala ya Msahafu ikiwa salama kabisa chini ya magofu ya nyumba yake iliyoharibiwa kaskazini mwa Gaza, akieleza hisia za kina na shukrani baada ya miezi ya mashambulizi.
Habari ID: 3481371    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/15

IQNA – Baada ya miezi kadhaa ya kufungwa kutokana na mashambulizi ya angani, Msikiti wa Al-Tawhid ulioko katika kambi ya wakimbizi ya Al-Shati, Gaza, umefunguliwa tena na sauti ya adhana imeanza kusikika kwa mara nyingine.
Habari ID: 3481366    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/14

IQNA – Sherehe ya watu wa Gaza kwa ajili ya kusitishwa kwa vita ni yao pekee, si ya Donald Trump, ambaye ametangaza kuwa atatembelea eneo hilo kuchukua sifa kwa kile anachokiita “tukio la kihistoria”.
Habari ID: 3481349    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/10

IQNA-Vita vya Ghaza na jinai nyingine zinazofanywa na utawala ghasibu wa Israel zimekabiliwa na msururu wa mashinikizo ya kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni ambayo yameufanya utawala huo ghasibu kuwa taifa linalochukiwa na kukataliwa duniani.
Habari ID: 3481334    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/05

IQNA – Idadi kubwa ya watu wameshiriki katika maandamano katika nchi mbalimbali kuonyesha mshikamano na Gaza na kulaani hatua ya Israel kuuteka nyara Msafara wa Meli wa Global Sumud uliokuwa umebeba misaada ya kibinadamu kuelekea eneo hilo a Wapalestina.
Habari ID: 3481319    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/03

IQNA – Hatua ya utawala wa Israeli kuzuia meli za Msafara wa Kimataifa wa Sumud imezua shutuma kali kutoka kwa serikali na mashirika ya kimataifa kote duniani.
Habari ID: 3481315    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/02

IQNA – Harakati za mapambano ya ukombozi wa Wapalestina, Hamas na Jihad ya Kiislamu, zimetoa matamko ya kulaani hatua ya Marekani kutumia kura ya turufu au veto kuzuia kupitishwa kwa rasimu ya azimio la kusitisha vita Gaza, wakisema kuwa hatua hiyo inachochea jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel.
Habari ID: 3481253    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/19

IQNA – Washiriki wa mkutano wa kimataifa wa wanawake uliofanyika Tehran wametoa wito wa kususiwa kwa kina kwa utawala wa Kizayuni, wakilaani vita vya mauaji ya halaiki vinavyoendelea dhidi ya Gaza.
Habari ID: 3481210    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/09

IQNA – Akielezea unyama unaoendelea kufanywa na utawala wa Israel dhidi ya Wapalestina, Mtaalamu Maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu maeneo ya Palestina yanayokaliwa kwa mabavu amesisitiza haja ya kukatisha mahusiano yote na Israel.
Habari ID: 3481187    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/05

IQNA- Maandamano yafanyika Uingereza kulaani  mauaji ya kimbari yanayotekelezwa na Israel dhidi ya Gaza Maandamano makubwa yamefanyika nje ya ubalozi wa utawala wa Israel mjini London, Uingereza kulaani mauaji ya kimbari yanayotekelezwa na utawala huo dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza.
Habari ID: 3481127    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/24

IQNA-Kiongozi mkuu Waislamu wa madhehebu ya Shia nchini Iraq, Ayatullah Sayyid Ali al-Sistani, ameelezea masikitiko yake makubwa kuhusu hali ya kibinadamu inayoendelea kuzorota katika Ukanda wa Gaza, hususan baa la njaa linalozidi kushika kasi, na kutoa wito kwa mataifa ya Kiarabu na Kiislamu kuchukua hatua za haraka kukomesha janga hili la kusikitisha.
Habari ID: 3481002    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/07/26

IQNA – Mwanazuoni wa ngazi za juu wa Kiislamu kutoka Iran amewataka viongozi wa Kiislamu na Kiongozi wa Kanisa Katoliki kushikamana dhidi ya mzingiro wa Israel huko Gaza, ambako njaa inazidi kupelekea janga kubwa la kibinadamu.
Habari ID: 3480992    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/07/24

IQNA-Kamanda mwandamizi wa Sarayal-Quds, tawi la kijeshi la Harakati ya Jihadul-Islami ya Palestina ametangaza kuwa, askari wapatao 40 wa jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel wameuawa au kujeruhiwa katika operesheni ya kijeshi iliyoratibiwa na wapiganaji wa Muqawama mashariki ya Ghaza.
Habari ID: 3480898    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/07/05

IQNA – Kocha wa klabu ya Manchester City, Pep Guardiola, ameelezea kwa uchungu hali ya mateso ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza, akisema ni jambo linalomuumiza sana kila anapofikiria yanayoendelea katika eneo hilo.
Habari ID: 3480823    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/06/11

IQNA-Katika hali ambayo, meli ya "Madleen" iliyokuwa imebeba misaada ya kibinadamu ilikuwa imekaribia Gaza, majeshi ya utawala haramu Israel yalishambulia meli hiyo katika hatua iliyotajwa kimataifa kuwa ni uharamia, na kuwateka nyara abiria wake na hivyo kuzuia misaada hiyo kufika Gaza.
Habari ID: 3480818    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/06/10

IQNA-Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa Linalowahudumia Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA) amezitaka nchi za Kiarabu katika Ghuba ya Uajemi kutenga tone tu la fedha zilizotajwa katika ‘makubaliano makubwa’ kati yao na Rais wa Marekani, Donald Trump, ili kusaidia wakimbizi wa Kipalestina wanaopambana kuendelea kuishi katika ardhi zao ambazo Israel imezikalia kwa mabavu na pia wale wanaoishi katika nchi jirani.
Habari ID: 3480762    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/05/30

IQNA-Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, katika mkutano na maafisa wa Makao Makuu ya Kanisa Katoliki Duniani, Vatican huko mjini Rome, ametoa wito wa kuchukuliwa hatua za haraka za kimataifa kukomesha uhalifu unaoendelea kutendwa na utawala katili wa Israel huku Gaza, na kuhakikisha misaada ya kibinadamu inafika katika eneo hilo lililozingirwa.
Habari ID: 3480732    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/05/24

IQNA-Shirika la Kimataifa la Uhamaji (IOM) limeripoti kwamba zaidi ya Wapalestina 97,000 wamehamishwa Gaza katika kipindi cha siku nne pekee, huku mashambulizi ya Israeli yakizidi kuwa makali katika eneo hilo lenye mateso.
Habari ID: 3480710    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/05/20

IQNA – Nchi wanachama wa Muungano wa Mabunge ya Nchi za Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (PUIC) zimetoa wito wa kuwekwa vikwazo vya kimataifa dhidi ya Israel, huku utawala huo ukiwa unaendelea na vita vya mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina katika ukanda wa Gaza.
Habari ID: 3480695    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/05/17